IFAHAMU HUDUMA YA FORGIVEN TO FORGIVE



FORGIVEN TO FORGIVE
Forgiven to forgive ni kikundi kinachoundwa na vijana wa kikristo kutoka madhehebu mbalimbali. Kikundi hiki ni matokeo ya maono aliyokuwa nayo bro. Laban Philimon Nzelela na baada ya kukaa nayo kwa muda mrefu tangu mwaka elfu mbili na kumi na moja,ilipofikia mwaka elfu mbili na kumi na tano(2015) kikundi hiki kikawa kimeanza lakini hakikuwa na jina mpaka kiliposhauriwa na mchungaji mmoja kuwa ni vyema kuwa na jina. Mwanzoni mwa mwaka huu FTF ikawa imeanza utendaji kazi wake rasmi mwaka huu 2016. Hii ni baada ya kupata watendaji kazi wa kudumu Ikiwa chini ya uangalizi wa BROTHER.
LABAN PHILIMON NZELELA.
Ikumbukwe mnamo mwezi wa sita mwaka 2015 forgiven to forgive ilianza kutekeleza maono yake kwa mkakati wa kutembelea makanisa mbalimbali na kutegemeza wachungaji.
Lengo kubwa au dhumuni  kubwa la kuanzisha  huduma  hii  ni kutaka sana watu waelewe  maana halisi ya NENO MSAMAHA na pia wajifunze kusamehe katika maisha yao ya kila siku MATHAYO 6:14  tukijifunza maisha halisi ya YESU KRISTO   ni maisha yaliyo tawaliwa na msamaha
*Pia huduma  hii imekusudia kuwainuwa watu kiroho na kimwili, tunapozungumzia kiroho  tunamaanisha watu wamjue kristo kiundani kwa mafundisho ya neno la MUNGU.
       =KIMWILI; YESU alipokuwa akiwafundisha makutano kwa muda mrefu ulifika wakati wanafunzi wake waka mwambia Bwana tuwaruhusu watu hawa wakajipatie chakula  lakin YESU alijibu wapeni ninyi Chakula   Kwa statement hiyo inadhihirisha  watu wahitaji kwa roho pia kwa mwili na si kwa chakula tu bali hata mali zetu.
*Lengo lingine ni kwafikia watu wasio jiweza kama YATIMA, WAJANE,WAZEE,WALEMAVU na pia WAGONJWA. na njia kuu ya kuwafikia watu hao ni by providing their basic needs 
  *Pia tuna lengo la kuandaa na kufanya semina mbalimbali  za NENO  la MUNGU  zitakazo fundisha watu kuhusu injili ya KRISTO NA MSAMAHA ULETAO UHURU WA NAFSI .....wakati mwingine hata kualikwa sehemu mbalimbali kwa ajili ya kufundisha neno la MUNGU 
*Pia kuwafundisha vijana wa shule za misingi, sekondari,Vyuoni na vijana wote  kuhusu maisha halisi ya kumjua MUNGU na UAMINIFU wake.
=Kuwafikia vijana wote wa maeneo yote hasa vijijini kwa ajili ya kuwafundisha NENO LA MUNGU
=Kufikisha NENO  la MUNGU kwa namna nyingi na tofauti tofauti  kwa mfano kuprint Tshrt   zenye  ujumbe wa  kimungu, pia vitabu vitakavyo fundisha kuhusu  IMANI, UPENDO, MSAMAHA, MAHUSIANO YALIYO SAHIHI MBELE ZA MUNGU na nk..........
=Kutembela makanisa mbalimbali kwa ajili ya kufundisha neno  la MUNGU  pia kuwategemeza wachungaji
=Kuwa na mikesha mbali mbali itakayo fundisha mambo mengi  kuhusu ukuu wa MUNGU .
=Kuwafikia wahitaji au makundi maalum katika jamii.

Pia Tunakukaribisha uweze kushirikiana na Forgiven to Forgive kuwafikia wahitaji.

Comments