FAMILIA NA JAMII

HAPO NDIPO UNAPOTOFAUTIANA NA MWENZAKO


Kioo huwa hakisemi uongo ila huwa kinaongeza sifa ambazo wakati mwingine huwa haunazo,usahihi au upungufu wa taarifa hutegemea aina ya kioo maana kuna vingine huonyesha mkono wa kushoto uko kulia na wa kulia uko kushoto.
Maisha ya wengine hawayezi kuwa kioo chenye taarifa sahihi kwako ila hukufanya ubadilike au uongeze kasi ya ufanyaji wa mambo yako,,,,,ila dah tofauti yako na mwenzio iko hapa.........................
Wakati wewe unapiga hesabu ya wapi utapata elfu ishirini ili ikamilishe laki moja kuna mwenzio tena yawezekana ni mshirika wako au ni mtu unayemuongoza kanisani au ofisini kwako huyo mwenzako anawaza atawasaidiaje watu wenye shida kwa kidogo alichonacho.
Wewe unapoomba Mungu akubariki uwe na nyumba,gari,familia nzuri ili uishi kama uko paradiso,wakitajwa wenye nazo na wewe uwepo tena unafunga na kufunga lakini mwenzio huyo jirani yako yeye aombapo huwakumbuka wenye uhitaji kama mayatima,wazee,wajane na walemavu tena huumia akiona hana namna ya kumsaidia hivyo muda wa kujiombea yeye hutumia kuwaombea wengine tena kwa machozi eeeeeeeeh! Mungu.


Tena huwa unanishangaza kwani kutoa kwako sadaka ni kama yule mtu akopeshaye maana hutaka sadaka yako irudi tena na zaidi , mmmmmh Fulani hakuelewagi pia lile neno unalopenda kulitumia kuwa Bwana atakupa vya kujaa na kushindiliwa hivyo sadaka yako isiwe bure loooooh! Unajua unatofautiana wapi na mwenzio,,,yeye hutoa kw a moyo wa kumshukuru Mungu na wala hatarajii Mungu ampe eti kwa kuwa ametoa bali hutoa kwa kuwa anampa aliyempa.Sasa aliyetoa unamkopesha kwa riba kweli!!! HAPO NDIPO UNAPOTOFAUTIANA NA MWENZAKO

Unalalamika hakuna anayekujali kanisani kwako hata ofisini  kwako,na muda wa ibada unapoisha wewe unaondoka tu hata husalimiani na watu,muda wa kazi ukiisha unaondoka hata huagi wenzio,kwenye masuala yanayotaka umoja wewe ni wa kwanza kukosoa,na kutoa mapendekezo mazuri ambayo hata huyafanyii kazi wewe ni kubwabwanya tu,,,,,,mwenzako sasa wakati unapoondoka yeye anabaki na kusalimiana na watu na kuagana nao,nani ajaliwe kati ya wewe na mwenzio,
Been unique is not avoiding others but by being blessings to others makes you to be unique and useful and that is possible when you associate with others.
Tena hili nalo limekufanya utofautiane na wengine si kwamba unachanua bali unafifia na kinachokufifilisha ni kwa sababu hujui unachotakiwa kukifanya kama ndo kitu ulichozaliwa ili ukifanye hivyo unaishi maisha ya watu wakati mwenzio anaishi kama alivyo ili akiinuka awe ameinuka moja kwa moja.

Huyu mwenzio si mkeo wala si mumeo
 bali ni kila anayekuzunguka katika jamii yako.
Nitaendelea kukwambia jinsi unavyotofautiana na mwenzako.
Bro.laban Nzelela

@ftfteam leader

Comments