KUWA KAMA ULIMBO KWA MWENZA WAKO
Nianze kwa kusema sifa ya ulimbo.
Ulimbo hukamata kile kitu ambacho hakijazidi uwezo wake wa kunasa, kwa
mfano ulimbo hauwezi kumnasa tembo kwani tembo uwezo wake ni mkubwa kuliko
nguvu ya ulimbo.
Wakati nilipokuwa nakua miaka ya tisini huko nilikuwa nikitega ndege
kwa ulimbo kwa kutumia kijiti ambacho nilikuwa nakichomeka karibu na sehemu
yenye maji ambako huwa ndege walikuwa wanakunywa maji na alipokuwa ndege ametua
kwenye hicho kijiti basi hakuweza kujinasua kwenye ulimbo.
Mfano
huu usikuchanganye sana ila kila upendo wa wawili hudumu ikiwa nguvu yao ya
kuvutana katika mioyo yao vimetoshana yaani mmoja ambaye amefanikiwa kunasa
moyo wa mwenzie.
Kwanini
uwe kama ulimbo kwa mpenzio??
Kuna
sababu nyingi zinazokufanya uwe kama ulimbo kwa mfano huu;
A:
Ulimbo huwa hausahau ikiwa kuna windo limenaswa kupitia huo ulimbo.
Ukiwa
na sifa hii,
1:
Hutaweza kumsahau mwenza wako
2:
Hutaweza kumshusha thamani yaani upendo wake kwako hautakuwa kitu cha kawaida
kwako.
B: Ulimbo
hupoteza nguvu kadri ya windo linavyojitahidi kujinasua.
It
is very true when you try hard to push away your lover from you he/she gets
tired and loose the first love when you agreed to be together and finally get
married.
This can separate you from your lover.
This can separate you from your lover.
C: ulimbo hupata nguvu zaidi unapopigwa
na jua.
Kama
utazikubali changamoto basi changamoto hizo zitakufanya kuwa mke au mume bora
baadae,na endapo utaonyesha kuzikimbia basi ni sawa na ulimbo kuutia michanga
na matope mengi ambayo yatapunguza uwezo wa kukaa na windo.
Simaanishi ulipo ni lazima
uendelee kuwepo bali itazame tena thamani ya moyo ulioamua kukupenda na
kukubali kuacha wengine na hata wakati mwingine moyo huo umesitisha kusoma au
kuanzisha mradi Fulani ili mradi tu mfikie kuoana kwanza hakafu hiyo mipango
itaendelea.
Nilikua sifahamu maana ya
kifungu kinachosema "upendo hautafuti mambo yake yenyewe" ziko
sifa kibao pale ukizisoma waweza ukaona kama ni hadithi tu ila nilikutana na
mama mmoja ambae alinambia kuwa yeye aliacha kusoma kwa sababu ya mchumba wake
ambae alitakiwa aoe haraka iwezekanavyo hivyo akaacha kuendelea na masomo na
kisha akaolewa na mpaka sasa ninavyoandika ana watoto wanne na wa kwanza
anaenda chuo,sambamba na hayo na yeye ana masters.
My
words to you if you have someone loving you know this he is just not there
because of your beauty or your handsome but he is there for a purpose, never
let him be alone in his darkest hour or her in her miserable situation. Just
stick there, he is sacrificing for you, so pray for her or him.
Ni
ukweli usiopingika hakuna kati yenu mwenye moyo wa chuma.
Bro.
Laban Nzelela
FTF
team leader.
Dedicated to my dear future wife and my dear readers.
Comments
Post a Comment