Nikisema hili neno kibuti japo
si rasmi lakini wengi tunalielewa,tena ndugu yangu Bedon Dickson hili neno
analifahamu mno na analitumia sana nyakati anapowasilisha mada hizi za kuacha
au kuachwa.
Kibuti linamaanisha ni kuvunjika
kwa uhusiano bila makubaliano ya wahusika,,unajua si kila wanaoachana basi
hugombana au huachana kimyakimya,hapana kuna wengine hukubali kuachana kwa moyo
safi bila kuweka kinyongo kwa mwenzako.kuna mazingira hutokea na watu huamua
kuachana kwa taarifa na tena na kuombeana wataombeana na kutakia mema huko
ambako kila mmoja atakwenda.
Lakini si hili neno
kibuti,ukisikia Fulani kapigwa kibuti huwa ni aibu,tena unaonekana wewe huwezi
aseeeee,kama una watani wako basi siku hiyo itakuwa ni kiyama cha furaha yako
maana malaika wa huzuni na aibu atakuwa amekushikilia,
,ubaya uko hapa apigaye
kibuti huonekana shujaa kuliko yule aliyepigwa kibuti maana kwake ataona
ametoka kwenye tanuru.
Kibuti hakihitaji
maelewano,unaweza pigiwa simu tu siku hiyo tena wewe bila kujua ukaanza,,; hello,baby
umenikumbuka asubuhi, miss you, love you,, enheee nambie mpenzi wa moyo (ukijisikia
kupenda mno)
Weeeeeeee !!!angalia jibu
hilo sasa
;aaaaah safi tu,(huku
amekunja USO),,mi naona tuachane tu na kuanzia leo usinipigie simu na namba
zangu futa kabisa.
Daaaaaaaah! tena nimekumbuka
mimi nilishapigiwa simu nikaambiwa hivyo sema sikua kweli katika mahusiano na
huyo binti ila alihisi natamani kuwa nae na nilipojaribu kumwambia Mimi ni kama
rafiki hakunielewa mpaka alipopata mbadala wa mvulana mwingine ndo akanipigia
hiyo simu.
Kibuti kinauma,ni kweli
kinakushushia heshima lakini wakati mwingine kinakufundisha na kukukomaza.
Kwanini usilie unapopigwa
kibuti???????????
Hii si rahisi hebu imeze kama
dawa chungu vile ili ikusaidie huko ndani.
A: Hukuendana na tamaa ya moyo wake
Si kama utakuwa unajifariji
hapana ila zingatia hili,"kila mke mwema alitokana na mwanamke aliyekuwa
na sifa za kuwa mke na si kila mwanamke aliyezaliwa na mwanamke aweza kuwa mke
mwema kwako"
Vivyo hivyo,"wanaume ni
wengi kuliko maelezo lakini mume mwema ni yule atakayekubali kuwa mume wa mtu
na wala si Wa kijiji"
Labda alikuja kwako kwa sababu
ulionekana ni aina ile aliyoitaka lakini alipogundua hapa sipo nitachemka
ikabidi aombe poooo!!!, she/he thought that you are just a sexy machine and not
a man/woman with a quality of been married.
B: Ulimuomba Mungu akupe mwema na huyo hakuwa mwema ndo maana kaondoka.
Ukielewa hapa hautajuta hata
kama muda umepoteza mshukuru Mungu acha kukunja uso kama Mzee,acha kuharibu uso
wako kwa machozi yasiyo na tija, au umesahau aombaye mkate hapewi jiwe bali
hupata alichoomba??
C: Unastahili zaidi kuliko alivyofikiri.
Nafikiri ulishawahi kusikia
baadhi ya watu wanasema mi siwezi kuwa na mtu Fulani kwa sababu anaonekana yeye
ni matawi ya juu,,,,huo ni msemo ambao huwafanya watu wajitoe kwenye
kinyang'anyiro hicho.
Simaanishi pesa hapana angalia
hadithi hii,"kulikuwa na kijana mmoja ambaye alivutiwa na binti Fulani
,hivyo akapanga namna ya kuwa karibu ili aweze kumnasa bahati nzuri alifanikiwa
kuwa karibu na binti tena ni ule ukaribu wa mtu na mpenziwe.lakini lengo
la kijana lilikuwa ni kumtumia na akishamtumia basi aachane nae.
Kadri ya ukaribu ulivyozidi
na mahaba kuongezeka kijana akaanza kusikia hukumu moyoni mwake kwani yeye
hakuwa na mpango wa penzi la dhati bali ni wizi kisha kibuti lakini
kwa kuwa msichana alionyesha penzi la dhati ,,jamaa akashindwa kuuficha ukweli
akamwambia kiukweli nilipokuona nilikutamani na nikapanga nikuumize na mbinu
zangu zimefanikiwa bado moja tu lakini hilo moja siwezi kulifanya na naomba
tusifike mbali tuwe rafiki tu,."
Anapogundua unastahili zaidi ya vile alivyokuona anakosa ujasiri wa kuendelea hivyo anaruka na kuliacha gari katika mwendo.
Anapogundua unastahili zaidi ya vile alivyokuona anakosa ujasiri wa kuendelea hivyo anaruka na kuliacha gari katika mwendo.
Pole kama yamekukuta na kama
hayajakukuta elewa haya mapema maana moyo wa mtu ni kichaka.
#ftfteam
Comments
Post a Comment