MAHUSIANO: KAULI SITA ZA KUEPUKA KATIKA MAHUSIANO BORA







Unapokuwa umeamua kuwaacha wote na kuamua kummamini mmoja tu ambaye huyo mnaweza mkafanya maisha
Mnaweza kuunganisha si yai nabegu ili kupata watoto tu Bali hata utafutaji wa maisha ili kiwa na future iliyo nzuri.
Ujue japo huwa tunasemaga akiniacha nitatafuta mwingine mioyoni mwetu huwa tunamaana tofauti na maneno,,.uhusiano wowote unapovunjika huacha maumivu hata kama ulikuwa ni wa kirafiki tu.
Mawasiliano ni jambo muhimu mno kwa kila nyanja ya maisha yetu.
Mawasiliano si kwa kutumia simu bali ni zaidi ya kupigiana simu au kutumiana jumbe fupi.
Mawasiliano ni mahusiano kauli uzitoazo huonyesha dhahiri mahusiano yako yakoje na watu au mtu unayewasiliana naye ,ukiongea kauli za kuumiza zinazosababisha maumivu ni dhahiri hivyo ndo namna mnavyohusiana.
Uti wa mgongo wa mahusiano ni mawasiliano na kila eneo au nyanja ya maisha yako kauli safi zisizoumiza zinahitajika ndo paulo katika nyaraka za timotheo anasema uwe kielelezo na anataja neno katika usemi.
Endapo yatavurugwa au hayatakuwa na kutiliwa mkazo basi kuna hatari kubwa yakaharibiwa,kufa au bora liende.
Wewe mwenyewe ni shahidi wakati ujenzi wa mnara wa Babeli kilichowabeba hata kufikia hatua ile ilikua ni mawasiliano.
Yaani lugha rafiki ndo iliwafanya wawe wamoja mpaka Mungu akaamua kuvuruga usemi wao.
Kwenye biashara yako kosa lugha rafiki kwa wateja wako hapo ndo utakapojua kwanini mwanga wa mwezi ni muhimu lakini haukaushi mazao.

Kwenye familia lugha ikichafuka hiyo sio familia ni genge la wababe.
Nchi ikikosa usemi unaoeleweka basi ujue hata kama mti wenye mwiba si rahisi kuupanda utageuka mwembe tu.
Kanisani usemi ukichafuka ndo utafahamu imani ya watu kwa Mungu wao.
Kadhalika katika mahusiano ya urafiki kuelekea uchumba hata ndoa inategemea sana lugha rafiki, lugha rafiki ni lugha isiyoumiza  upande wowote.
Unaweza kuchagua mwenyewe ipi itakufaa na ukaonekana ni wa busara mbele ya nwenzi wako.
Uchaguzi ni wako kuchukua kiatu cha wazi au cha kufunika,kutangaza mambo yenu ya mahusiano au kuyatafutia ufumbuzi wako mwenyewe.
Uchumba,urafiki au ndoa inayokosa mtu confidant ni hatari sana
Mume anahitaji mke confidant,vivyo hivyo mke anahitaji mume confidant yaani mwenye kifua.
Lugha zenye chembechembe za kuumiza husababisha utengano wa mioyo kati ya wapenzi.
Kuna kauli au maneno ambayo unatakiwa kuwa makini nayo wakati yanatumika au yaepukwe ili kuepusha kuumizana.
Kauli hizi huonyesha muyumbo au kifo cha mahusiano
Tuziangalie kauli sita za kuepukwa ili kuwa na mahusiano bora.
Hebu zitazame kwa umakini hizi kauli halafu utanambia hata kama zinaonekana ni za kawaida lakini zimebeba sumu Kali inayoweza kuleta giza na ukungu wa huzuni katika mahusiano yetu
Kila mtu anapenda afurahie na ajisikie ni yeye tu katika dunia hii tena kama ni mkeo  ndani ya ndoa hata ukijaza account yako ya insta au Facebook kwa kumsifia sitashangaa maana hiyo ni lugha tamu.
Weka hata kwenye wallpaper yako picha ya mama mtarajiwa au baba,,save jina zuri hata akijaribu kujibipu anaona jina my cute,my queen, wala si my headache

1: Kama ni hivyo mi nitashindwa.
Kauli hii huweza kujitokeza endapo kuna mmoja kati ya wapendanao anaonekana kutoeleweka,au mmoja anashindwa kumwamini mwenzie hivyo hutishia kuvunja uhusiano
Utasikia tabia zako sizielewi elewi,mbona hufanyi kama tulivyokubaliana kama ni hivyo mi nitashindwa na tutaachana.
Hakuna jambo baya kumtishia mwenzio ikiwa tayari ameshajikita kwako,hii huzaa uchungu,hujenga maumivu kwa mwenza wako.
Mimi naamini kuna maneno yanaweza tumika kama mbadala ya kauli kwa mfano tabia yako haipendezi hivyo iache.
Na si kutishia kuvunja mahusiano pasipo kuzungumza kipi ni kibaya kati yenu.
Na hata kama itatokea mmevunja mahusiano ya uchumba wenu itakua ni kwa sababu zenye mashiko labda mkioana si rahisi kupata mtoto kutokana na sababu za kibailojia,na hapa ina maana kila mmoja atajua kwanini mnaachana na kuridhiana kutoana mioyoni kabisa.
Najua urafiki au uchumba si ndoa kama unaona hauendani au unaona huyu si mtu sahihi na labda ulikurupuka kwenye kuamua kutokana na labda ulichokuwa umepitia kilifanya usifikiri kwa makini ila ulimpa nafasi ili kuziba pengo na sasa unajiona umerudi kwenye ufahamu wako,ongea kwa uzuri naamini suluhisho litapatikana .
kuliko kutishia kwa maana unajuta kuwa nae na unamtafutia sababu ya kuachana nae,sababu unayo tayari tell the truth.

2: kwa sasa tusizungumzie mahusiano
Yaani mko kwenye mahusiano tayari lakini mmoja wenu anasema tusizungumzie mahusiano kwa sasa.
Why; shule imebana,kazi imebana sana
Hivyo nashindwa kugawa muda kati ya kazi na mahusiano kwa hiyo tafadhali tuache kwanza.
"Kuna rafiki yangu alinifuata kipindi tuko chuo mimi mwaka wa pili na yeye wa kwanza na kunambia kwamba anamsichana amempenda sana hivyo nimshauri kama vipi awe nae.Baadae ya kumuuliza maswali kadhaa nikamwambia sawa kuwa nae.
Lakini baada ya msichana huyo kumaliza chuo na jamaa akawa bado ndipo akamwambia', kwa sasa tusizungumzie mahusiano'"
Kauli hii ni mwanzo mzuri wa kuumiza moyo wa mtu na pia ni njia isiyo na miiba iendayo kwenye kuvunja mahusiano.
Hapa yawezekana amezungumza kwa ufahamu wake mdogo tu na wala hana mawazo ya kuvunja,,,au ana mawazo ya kumaanisha kuvunja hivyo anatafuta mbinu ya kukuweka kwenye mazingira ya kukuacha hivyo unaandaliwa kisaikolojia ili akichomoka uwe umeshazoea.
Kuna watu wako bize na bado wana jenga mahusiano yao vizuri tu.

3: Sijui Itakuje?

Hii kwetu wanaume kwanza lazima uelewe hupati mke eti kwa kuwa unahela ,,pesa hazimfanyi mwanamke anayejielewa akatamani kuishi na wewe,,,
Wanawake wanapenda wanaume wanaojielewa, mwanaume anayeulizwa na kujibu kama kazaliwa na jibu hilo,sio unaulizwa sherehe itakuaje?,unasema hujui,,kaaaah!!!
You have to straight know that you will soon be the head of the family or you are in already so make your woman been proud of u
No matter you don't have enough for today but as long as you are bold hustling,am sure her heart is yours.
Na wanaume hupenda mke mwenye fikra pevu,jibu la sijui huwa linatoa sura ya mke mwema na kuweka mke asiyejielewa.
Huleta wasiwasi kwa mwanaume hasa mwenye malengo makubwa anapoona hufanani na yawezekana si kweli ila unakosa umakini.

4: Umeanza kama kawaida yako 

Hapa huonyesha moyo wa mmoja umekuwa sehemu ya kuhifadhia vitu vibovu.
Mfano rahisi pita kwenye dampo na ukakuta hali ya hewa safi,kisha chukua kijiti na fukua kwenye uchafu hapo harufu itakayotoka hapo ni hatari.
Ndivyo moyo wa mpenzi anayehesabu makosa hivyo ukikosa haanzi na la leo bali la mwezi uliopita mpaka afike la leo si chini ya lisaa limoja ni lawama tu.
Hii mbaya mno kwani huonyesha uwezo hafifu wa kusamehe na hivyo kumfanya mwenzio ajisikie ni mkosaji asiyestahili kusamehewa.
Hata kama uko kwenye ndoa tayari chunga sana hili eneo utatia tope kwenye kiti cha harusini halafu ndiwe unayetakiwa kutoa nasaha ,utainukaje wakati ushachafuka aseeee.
Kila mwenye kidonda anajua kukilinda ili kisisumbuliwe na nzi au kutoneshwa iweje wewe usiweze kulinda mahusiano yako.

5:"Kama vipi basi",
Hii husemwa si kwa lengo la kuridhika bali ni kama kero hivyo unaamua bora liende lakini si kwa uzuri.
Hii inaleta kutu kabisa kwenye mahusiano.

6: Lazima Asikie Uchungu wa Mke’
Msichana anasikika akijisemea kwa rafikize kwamba ili mchumba wake aone uchungu wa kuoa basi inabidi agharamike katika kutoa mahari ndefu.
Mbaya zaidi katika vimazungumzo vya kubadilishana mawazo na mtarajiwa wake anaanza tena,"mimi ni mwanamke mzuri,na nimesoma hivyo mahari yake hapa inabidi ujipange,na ninavyojua wazazi wangu na hata kama ningekuwa mimi ndo mzazi mwanangu angeolewa kwa gharama".
Eeeeh! Ni vyema lakini hata ikisemwa kwa utani bado inapenya kwani huo si utani bali ni mzaha na mzaha hutumbua jipu.
Kama wewe umesoma hivyo unatakiwa uposwe kwa pesa ndefu ungeolewa na elimu yako kama inawezekana.
Kama msichana unajielewa hii si kauli ya kuzungumza popote pale ulipo.
Bro.labannzelela.
Founder ftf.

Comments