SOMO: KIELELEZO CHAKO KIKO WAPI?
NA: Bro Laban Nzelela
Sehemu ya kwanza.
Sehemu ya kwanza.
Maandiko
yamenena hivi,*mtu yeyote asiudharau ujana wako Bali uwe
kielelezo........"
Mi hata sitaki kuzunguka ila naomba niseme hili,kwa hali tuliyonayo sasa hasa kanisa au waaminio wokovu (kuzaliwa Mara ya pili), ni hali ambayo imechangamka mno tofauti na zamani maana vijana tumekuwa na mwamko wa kumtumikia Mungu tena tunajitoa hasa.
Mi hata sitaki kuzunguka ila naomba niseme hili,kwa hali tuliyonayo sasa hasa kanisa au waaminio wokovu (kuzaliwa Mara ya pili), ni hali ambayo imechangamka mno tofauti na zamani maana vijana tumekuwa na mwamko wa kumtumikia Mungu tena tunajitoa hasa.
·
Miaka ya nyuma ilikua
nadra kukuta vijana wamependeza tena wanamikato ya hataree wanachapa injili
lakini kwa sasa tumevunja record maana idadi imeongezeka na watu wamepanda
mori(sio ile ya kimasai),yaani wameamka.
·
Mbali na kuwa wimbi
la vijana wanaokimbilia kwenye huduma linaongezeka lakini mvuto Wa huduma nao
unapungua,heshima na maadili ya kikristo hawaeleweki ni kama mlevi ambaye akiwa
hajanywa huwezi elewa kama ni mlevi ila akinywa ni hatareee.
·
Labda mwenzangu
waweza ukawa na jibu? eeeeeh! Kama unalo tusaidiane kukumbushana.
Yaani ile hofu na heshima iliyotajwa na Yesu kuwa tutaipata tukimtumikia Mungu bado iko mbali na si rahisi kuifikia,Napojiuliza naona kuwa vijana wengi tunapoteza sura na ladha ya wokovu hata kama tunakiri tunamtumikia Mungu aliye hai .
Yaani ile hofu na heshima iliyotajwa na Yesu kuwa tutaipata tukimtumikia Mungu bado iko mbali na si rahisi kuifikia,Napojiuliza naona kuwa vijana wengi tunapoteza sura na ladha ya wokovu hata kama tunakiri tunamtumikia Mungu aliye hai .
·
Upentecoste
naufananisha na mbuzi anayefahamu mahali ambako kuna maji au mnyama yeyote wa
kufugwa pindi anaposikia kiu hata kama utamzuia ni lazima ataenda na kunywa, ndivyo
tulivyo sas a *wenyeji umezidi sana kiasi kwamba tunaona kawaida*.
·
Ufunuo aliposema
mmemkaribisha mbele tena mmempa kiti cha mbele akakaa,!!! najiuliza alikuwa
anamaana gani?????.
·
Okay tufanye hivi kwa
Leo wewe kama ni kijana na unatumika jitahidi usiwe kila kitu, kuwa na mtu
aliyekutangulia tena itafaa awe wa zamani kidogo ili ujifunze maadili ya
kiktisto hii itakuwa rahisi kwani utakapokuwa unaongezeka katika viwango vya
utumishi na malaumu nayo yatakuwa yanapungua.
·
Usidharau hili tena
unapoambiwa hili vazi sio tii,namna ya utumishi wako kuna vitu punguza kubali
kwani *kabla ya huduma unayotoa maisha yako ni huduma tosha*,mwana mzuri ni
yule anayekubali maonyo na mafundisho.
Kielelezo kimepotelea wapi?
Hapa ndo shida sasa,kama hujajua unatatizo basi ni ngumu kulitatua tatizo.
Kama huamini muulize daktari ambaye anahudumia mgonjwa asiye na uwezo wa kuzungumza,hiyo diagnosis daktari anapata kazi sana kumwandikia mgonjwa wa namna hiyo.
Hata mwana wa nabii aliyedondosha shoka aliulizwa na Elisha limedondokea wapi?, kujua tatizo na chanzo cha tatizo ni robo tatu ya suluhisho la tatizo lako.
Hapa ndo shida sasa,kama hujajua unatatizo basi ni ngumu kulitatua tatizo.
Kama huamini muulize daktari ambaye anahudumia mgonjwa asiye na uwezo wa kuzungumza,hiyo diagnosis daktari anapata kazi sana kumwandikia mgonjwa wa namna hiyo.
Hata mwana wa nabii aliyedondosha shoka aliulizwa na Elisha limedondokea wapi?, kujua tatizo na chanzo cha tatizo ni robo tatu ya suluhisho la tatizo lako.
Kuna mambo lazima uwe makini nayo hasa
tunapokusanyika vijana katika makusanyiko mbalimbali,kwani wengine
hukisanyika kwa lengo tofauti na lile lililowakusanya kulingana Yale
wanayoyatamani.
HAPA NDIPO ULIPOPOTEZA KIELELEZO CHAKO.
1.
Makusanyiko ya vijana tupu.
Hata mwana wa suleimani alipopuuza
ushauri wa wazee na kuamua kuukubali wa vijana wenzie tunaona madhara
aliyoyapata.
Waliotangulia ni hazina yetu hata kama
wanaonekana kuishiwa mbinu,samweli hakumdharau Mzee Eli hata kama ilionekana
Eli ameshachoka kiroho na kimwili hata Mara
baada ya kuambiwa na Mungu bado alimheshimu.
Kwenye makusanyiko mengi ya vijana
usipokuwa makini unaweza kupoteza kielelezo chako maana wote mko kwenye hatua
moja ya ujana.
Mfano rahisi tu usiyohitaji shule ni
kwamba asiyeoa hatakiwi kuombwa ushauri na mtu anayetaka kuoa,unataka kuoa
tafuta watu ambao wamekaa kwenye ndoa angalau miaka mitano na kuendelea.
Vijana wengi wanatumia uzoefu wa miaka
miwili au mmoja katika huduma halafu wanajiona wamekua.
2.
UNAJILEA AU UNALELEWA (you got a spiritual
father?)
Kama huna baba wa kiroho nakuhakikishia
utayumba tu,kwani baba wa kiroho yupo kukuongoza na kukufundisha ili kuufikilia
wito wako lakini kabla hujafikia huko ni lazima ulelewe vizuri.
Nikwambie siri hii, baba wa kiroho
huwa hasemi ndio kwa kila unalofanya.
Baba wa kiroho si mshauri wako tu hapaba bali anawajibika katika kufanikiwa na kushindwa kwako.
Wengi wanawashauri na wala si baba kiroho,japo wao wanaamini ni baba zao kiroho.
Baba wa kiroho si mshauri wako tu hapaba bali anawajibika katika kufanikiwa na kushindwa kwako.
Wengi wanawashauri na wala si baba kiroho,japo wao wanaamini ni baba zao kiroho.
Note; If you are spiritual father all he can say is yes then he is not your spiritual father, he is just encouraging you and once you fail he will not be answerable.
3.
KIPI CHA KWANZA KATI YA MUNGU NA HUDUMA KWAKO.
Kuna mtu aliwahi kusema hivi,"nafasi yako au cheo chako kanisani au kwenye vikundi vya kanisa havina nafasi katika mahusiano yako na Mungu"
Kwa kusema hivyo si kama hakutambua umuhimu wako katika nafasi hiyo bali alitaka tutofautishe maisha yetu na Mungu na Maisha yetu katika vyeo vya kwenye huduma,unaweza ukaitwa majina mengi kwenye vikundi unavyoongoza lakini hayo hayasaidii kuboresha uhusiano wako na Mungu.
Ukikosea kwenye kipi kianze kati ya Mungu na huduma basi kielelezo ni ngumu kukipata.
Kuna mtu aliwahi kusema hivi,"nafasi yako au cheo chako kanisani au kwenye vikundi vya kanisa havina nafasi katika mahusiano yako na Mungu"
Kwa kusema hivyo si kama hakutambua umuhimu wako katika nafasi hiyo bali alitaka tutofautishe maisha yetu na Mungu na Maisha yetu katika vyeo vya kwenye huduma,unaweza ukaitwa majina mengi kwenye vikundi unavyoongoza lakini hayo hayasaidii kuboresha uhusiano wako na Mungu.
Ukikosea kwenye kipi kianze kati ya Mungu na huduma basi kielelezo ni ngumu kukipata.
4.
KUCHANGANYA WAGONJWA.
Kinachotoa umakini na umahiri kwa daktari
yeyote ni kuchanganya matibabu kwa wagonjwa,wewe mwenyewe ni shahidi kuna
oparesheni zilikosewaga baada ya mgonjwa aliyetakiwa kupasuliwa goti
akapasuliwa kichwa na yule wa kichwa akapasuliwa
goti,kilichotokea baadae ndicho kiliwashusha thamani madaktari.
Wewe ni kijana na unafundisha sana vijana mpaka imefikia unatumia lugha zile za vijana,hapo si shida maana ndo mahala pake..
Tatizo linakuja unapochanganyiwa wagonjwa yaani watu wa kuwahudumia unapewa kanisa zima kwa mfano na kwa kuwa umezoea vijana jitahidi usiwape kanisa dozi za vijana endapo utachanganya madawa basi ujue unaleta madhara.
Wewe ni kijana na unafundisha sana vijana mpaka imefikia unatumia lugha zile za vijana,hapo si shida maana ndo mahala pake..
Tatizo linakuja unapochanganyiwa wagonjwa yaani watu wa kuwahudumia unapewa kanisa zima kwa mfano na kwa kuwa umezoea vijana jitahidi usiwape kanisa dozi za vijana endapo utachanganya madawa basi ujue unaleta madhara.
You are not qualified so God is just trying to prone you.
Itaendelea………..
FTF team leader
FTF team leader
katika Yote tunahitaji msaada wa Mungu atusaidie tujue yapi mapenzi na makusudio yake kwewtu
ReplyDeleteHakika
DeleteAmen
ReplyDelete