Unahitaji
mshauri ‘mentor’ akusaidie kufika kule unapopaswa kufika
Pale unapohitaji kufika kamwe huwezi kufika peke yako ni lazima upate
mentor ambaye atakuwa anakusaidia kukuonyesha njia sahihi ya kupitia. Kama
hauna mentor wa kukuongoza, kukushauri na kukusaidia utaangaika kila siku
kwenye jambo lile lile na bado hautaona mpenyo.
Ukweli ni kuwa hakuna aliyezaliwa na maarifa na kufahamu kila kitu na
ndio maana kila siku na kila saa tunahitaji kujifunza ili tuweze kupata maarifa
ya kutusaidia.
Unahitaji mentor kwa kuwa kuna mambo mengi sana huyajui kabisa
ila huyo mentor atakusaidia kuyajua, atakushauri na hata kukukosoa unapokosoa
ili uwe kwenye njia sahihi.
Ukisoma kwenye biblia utaona watu wote waliofanikiwa katika huduma, na
hata maisha ya kawaida walikuwa ni watu waliokuwa wakijifunza na walikuwa na
watu ambao walikuwa wakufunzi wao na kila mara walikuwa wakiketi chini yao na
kujifunza kwao.
“chui huwa anazaa chui mwenzake (a tiger will give birth to a tiger)”
Timotheo na Tito walitumia muda mwingi kujifunza kwa Paulo kabla
hawajaanza kufanya huduma (kabla hujaanza kufanya hiko kitu tafuta kujifunza
kwa mtu ambaye tayari alikifanya au anakifanya), kabla hujaanza kupita hiyo
njia unayotaka kuipitia tafuta kujifunza kwa waliowahi kupita hata kama
hawakufika watakuwa na jambo tu la kukusaidia na linaweza kukusaidia usikwame
kama wao walivyokwama.
Elisha alitumia muda mwingi kujifunza kwa Eliya kabla hajawa Nabii
kushika sehemu ya Eliya (mkufunzi wake) na fuatilia utagundua kuwa muujiza wa
mwisho wa kufanywa na Eliya ndio ulikuwa muujiza wa kwanza kufanywa na Elisha
wa kuyapiga maji na vazi na kugawanyika na kufanya njia ya kupitia.
Joshua alitumia muda wake mwingi kujifunza kwa Musa kama mkufunzi wake
na maandiko yanaonyesha kuwa Yoshua alifanya vizuri sana na hata alipokuwa
anaukabiri mto Yordan alikuwa suala gumu sana kuugawanya mto huo watu wapite
kwa kuwa alishawahi kushuhudia mkufunzi wake akigawanya bahari ya shamu.
Unahitaji kujifunza kwa waliokutangulia, tumia muda wako mwingi kukaa
nao kuna mambo mengi sana watakusaidia kuyajua.
Unadhani kwa nini Mungu alimpa fursa Daudi kutoka porini kuchunga
kondoo na mbuzi na kumpeleka kuwa mpiga kinubi kwa mfalme? Bila shaka Mungu
alikusudia Daudi ajifunze mifumo na
taratibu na mambo ya kifalme ili akiwa mfalme isije kuwa taabu.
Kama unataka kuja kuwa mwanasiasa mkubwa tafuta sana wanasiasa
ujifunze kwao, soma na fatilia habari zao, mifumo ya maisha yao, jifunze
madhaifu na mazuri yao kabla haujafika, hii itakusaidia kipindi unafanikiwa
nawe kuwa utakuwa unauzoefu.
Hata Mungu amuinui mtu tu kutoka shambani na kumpeleka Ikulu moja kwa
moja, huwa anamuinua na kumpeleka karibu na watu wa mifumo kwanza ili ajifunze
kwanza na akishaona amefuzu ndipo anamuingiza kwenye mifumo. Na ndio maana
Yusufu aliuzwa kwa Potifa ili ajifunze namna ya kuwa kiongozi katika nafasi za
juu. Pale Mungu anapokuweka si bure ni lazima ujifunze kujifunza kabla
hajakuinua kukupeleka ngazi nyingine.
Unapokuwa chini na hujui hata hatua ya kufanya ili usonge mbele muombe
Mungu akupe mtu sahihi atakayekusaidia kutoka katika hilo eneo.
Mara zote ni lazima ufahamu kuwa unajifunza kwa kuwa kuna ujinga unao
na ujinga huo unatoka pale tu unapojifunza.
nice
ReplyDelete