HATARI ILIYOPO KATIKA MATUMIZI YA BIBLIA ZA MITANDAONI (SOFTWARE)
Biblia
ni neno la Mungu lenye uhai. Neno la Mungu ni pumzi ya Mungu aliyompulizia
mwanadamu alipoumbwa pale bustani ya Edeni.
Kila andiko
lenye pumzi ya Mungu lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na
kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki. Ili
mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema 2Timotheo
3 :16-17.
uhai wa mwanadamu umejengwa
katika uhalisia wa neno la Mungu la kweli, Maisha ya mwanadamu yanaongezeka na
kukua kwa sababu ya lile la neno la Mungu lilitamkwa kwa mwanadamu.
Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu
wako, kwa bidi, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo Kumb 28:1
Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani
mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda
sawasawa na maneno yote yaliandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia
yako, kisha ndipo utakapositawi sana. Yoshua
1:8
Kufanikiwa kwa njia yako katika Maisha
yako iko katika kuisikia, kutunza kuyafanya maagizo yote ambayo Bwana, Mungu
wako amekuagiza na huko kunakufanya usitawi sana.
Kusitawi kwako kupo katika
kulitafakari/ meditate neno la Mungu na kulifanyia kazi katika Maisha yako.
Neno la Mungu lina uwezo wa
kufanikisha Maisha ya mwanadamu
Kulisikia neno la Mungu na
kuyatunza maagizo yaliyo katika neno la Mungu kunaleta baraka za Mmungu.
Kulitafakari na kuangalia kutenda
sawasawa na yaliyoandikwa humo kunafanikisha njia yako na kukustawisha
Neno la Mungu lina nguvu ya
kumuinua mtu kutoka kwenye hali mbaya hadi kwenye hali nzuri ya kiuchumi,
kiafya, kiufahamu n.k.
Neno la Mungu lina uwezo wa kumpa
mwanadamu akili na ufahamu wa kuamua mambo magumu
Tunaishi
kwa sababu ya neno la Mungu.
Neno la
Mungu ni jambo linalopingwa wakati wote,watu wote wasiamini, mahali pote pa uso
wa nchi ni kwa sababu ya msingi kuwa hizi ni falme mbili,
Kuna wimbi
kubwa sana la mabadiliko ya sayansi na teknolojia ambalo linaikumba jamii ya
leo, siku za leo hata vipindi vya darasani viko online na assignment
zinafanyika online.
Hali hiyo hiyo iko hadi katika
kanisa kila jambo liko kwa kielektroniki kuabudu, neno la Mungu hata kutoa
sadaka ni online.
Mada yangu kubwa leo ni kutaka
kukuonyesha kwa sehemu ndogo tu hatari iliyopo katika kutumia Biblia za kielektroniki/softcopy/software
Bible
Biblia za kielektroniki ni zile biblia
za simu, computer n.k ambazo wakristo wengi leo wanaweza kuzibeba kwa sababu
hazina msigo mzito tofauti za kawaida ambazo kuzibeba zinahitaji nguvu ya ziada
siku za leo.
Makala haya ni tafiti ndogo
niliyoifanya kwa muda fulani ili kupata ufahamu juu ya jambo hili japo bado
halijakamilika kwa utandani kutokana na wakati bali nimependa tushirikishane
kidogo kisha tuendelee mbele zaidi.
Ufalme wa shetani siku zote
haupendi kuona wala kusikia kuwa mtu aliye katika ufalme wa Mungu Jehova
amefanikiwa ndio maana kila jambo linaweza likafanyika ili kuzuia na kuharibu
mambo mema
Katika
kizazi cha sasa tunajua kuwa maisha yetu yanaendeshwa na sayansi na teknolojia
kwa sehemu kubwa. Vivyo hivyo hata ubunifu na matumizi yake kila siku yanakua
ni kwa sababu ya msingi ya wakati wa kanisa tulio nao ni wakati wa kuongezeka
kwa maarifa.
Tuko kwenye
kipindi cha taadhari sana na uangalifu mkubwa sana
Yako mambo
machache nataka nilete kwako kuhusu mada yangu ya hatari ya matumizi ya Biblia
za mitandaoni.
Neno la
Mungu linapokuja kwenye maisha yako inategemea sana na nguvu ya yule anayeleta
hilo neno la Mungu, wengi wa wahubiri wa leo ni wale wanaotumia maarifa yao
katika kutafakari neno la kweli la Mungu si kwa nguvu iliyofunuliwa kwetu na
Roho mtakatifu.
Wengi
wa waalimu au wahubiri wa neno hilo la Mungu ni wale wanaona kuwa njia zao au
matendo yao ndio bora kuliko ya mwingine kwa maana kuwa kile anachokifanya ndio
ni kizuri kuliko cha mwingine. Wengi ni wale wanaotaka kufanya ili wengine
waone nini nafanya au na mimi naweza kufanya wengine waone na mimi naweza.
Hata hizo
biblia zetu za kwenye simu au ku install kwenye computer na vifaa vingine kama
hivyo waasisi wengi hawana ile nguvu ya Mungu ya kweli inayoweza kumbadilisha
mtu bali ni kufanya ili wengine waone au kupata faida za kimtandaoni japo kweli
wapo wengine ambao Mungu Jehova anawatumia kusema na maisha yetu.
§ Kutumia Biblia kwenye simu au computer au kifaa chochote
chenye uwezo wa kuhifadhi Biblia haikupi nafasi ya wewe kukaa na kutafakari
lile neno kwa undani
Mara nyingi
matumizi yake yanakuwa ya mchanganyiko na mambo mengine mfano halisi kwenye
simu utakuta unasoma Biblia huku unatuma text kwenye mitandao au mtu mwingine mambo
kama hayo hayakupi bidii ya kutunza na kuyafanya yale unayoagizwa.
Wimbi
kubwa la vijana hawaoni shida kwenda ibadani na kuchat katika mitandao mbalimbali
ya kijamii wakiwa ibadani
Kuna siku
nilihudhuria ibadani mchungaji kiongozi alitoa onyo kwa wale wote wanao chat
ibadani kwa kisingizio kuwa wanatumia Biblia kwa njia ya simu.
Jambo
hili linaweza kusababisha kupunguza thamani ya Mungu ndani ya mtu kwa sababu
concentration kubwa iliyopo ni kwenye mitandao sio kwa Mungu

Kusikia
kwa bidii kile kinachozungumzwa kwenye hilo andiko na kutunza kuyafanya yote
kunakupa baraka.
Ufunuo 1 : 3 heri asomaye na wao
wayasikiao maneno ya unabii huu, na kuyashika yaliyoandikwa humo ; kwa maana
wakati u karibu
§ Mfumo wa ulimwengu wa giza kuamua kupoteza neno la Mungu
katika maisha ya mwanadamu.
Kuna mifumo
mingi inayotumika kuharibu maisha ya walioamini hasa kumfanya aendane na
wakati.
Mfumo
huu umeandaliwa ili kulipoteza kabisa neno la Mungu kwa mwanadamu, leo teknolojia
imetusaidia kufanya mambo mengi kwa urahisi kabisa na hata kuona kubeba Biblia ni mzigo mzito hatimaye katika fahamu
itajengeka hakuna umuhimu wa kutumia Biblia, maamuzi yatakayotokea hapo ni kuamua
kuiacha kabisa na kuendelea kutumia simu zetu kama njia rahisi.
Biblia
inatukumbusha kuwa kama wakristo watu tulionunuliwa kwa damu ya thamani pale
msalabani inatupasa kuukomboa wakati maana ni zama za uovu.
Siku za
nyuma kidogo mtu akienda ibadani anaweza kubeba Biblia na diary kwa kwa ajili
ya short notice leo mkristo anaweza kwenda ibadani akiwa na simu tu kisha
akatumia kama biblia na diary kwa wakati mmoja.
Kumbuka
hiyo softcopy ambayo inaweza kuondolewa kabisa na kutoweka kwa hiyo ikitoweka
kwenye vifaa vyako na Biblia hauna itakuleta kwenye ombwe kubwa sana.
sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza
ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia; Ebrania 2 :3
Uwe mwangalifu
sana na hizo software unazotumia zisije kugharimu maisha yako. Tumia neno la
Mungu uhalali kabisa.
Wapendwa
wangu tuliochaguliwa na Bwana tufahamu kuwa tuko kwenye nyakati za mwisho za
unyakuo ni kipindi hiki ndio maarifa kila kukicha yanaongezeka kila siku jambo jipya litokea.
Unapotumia
tafsiri mbalimbali za Biblia ili kupata maana iliyokamilika usitekwe sana na
mambo mengi yanayoendelea bali uwe kwenye kusudi kamili la wewe.
Jihadhari
mteule uwe macho Bwana wako anakuja
Mungu
na akubariki sana
joshua dwende
0719 787 952
Comments
Post a Comment